DAKTARI DARAJA II (MEDICAL OFFICER II)
Employer: Wizara ya Afya
Salary Scale: TGHS E
Posts: 23
Closing Date: 18 Jul 2026
Duties & Responsibilities
i. Kufanya kazi zote za matibabu hospitalini zinazohusiana na magonjwa mbalimbali katika fani husika yakiwemo magonjwa ya watoto, magonjwa ya akina mama na upasuaji wa kawaida na dharura.
ii. Kutoa na kusimamia elimu ya afya pamoja na kuboresha afya ya jamii katika wilaya na mikoa au eneo la kazi.
iii. Kutunza takwimu na kuzitumia kama inavyoonekana katika mifumo.
iv. Kuchunguza, kufuatilia na kuzuia milipuko ya magonjwa.
v. Kutayarisha elimu ya kujiendeleza ya watumishi wa afya.
vi. Kusimamia na kuelekeza watumishi walio chini yake.
vii. Kubuni, kuendesha na kutathimini utafiti na kusambaza matokeo
viii.Kubuni na kutayarisha mikakati ya kuinua ubora wa huduma ya fani Yake.
ix. Kuandaa mipango na makisio ya bajeti ya huduma za afya
x. Kushiriki, kuhakiki na kuboresha huduma za afya( Medical audit and quality improvement)
xiv. Kuandaa mipango na makisio ya bajeti ya huduma za afya
xv. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.
Qualifications
Kuajiriwa wahitimu wenye shahada ya Udaktari kutoka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali. Wawe wamesajiliwa na Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika).
